Rais Xi Jinping wa China leo amezungumza na wanaanga wawili waliomo kwenye maabara ya anga za juu ya Tiangong-2 katika Kituo cha Kudhibiti Usafiri wa Anga za Juu cha Beijing.
Rais Xi amewajulia hali wanaanga hao na kuwataka waendelee na juhudi na kushirikiana ili kukamilisha majukumu ya baadaye bila ya matatizo.
Wanaanga hao, Jing Haipeng na Chen Dong walianza safari ya anga za juu kwenye chombo cha Shenzhou-11 tarehe 17, Oktoba, na kuingia kwenye maabara ya Tiangong-2 tarehe 19, Oktoba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |