• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya kuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa kupambana na utapiamlo

    (GMT+08:00) 2016-11-10 09:26:37

    Wataalamu wa lishe zaidi ya 100 kutoka nchi mbalimbali dunani watakutana mjini Nairobi wiki ijayo kutathmini maendeleo yaliyopatikana katika kupambana na utapiamlo duniani.

    Mwandaaji wa mkutano huo Bw. Schuyler Thorup amesema mkutano huo una lengo la kuweka mpango wa kuhimiza maendeleo ya kazi kuhusu lishe, maji na usafi, kilimo, afya, maendeleo ya utotoni, elimu na jinsia.

    Bw Thorup amesema kila mwaka utapiamlo husababisha vifo vya watoto takriban milioni 3 wenye umri chini ya miaka mitano, na kuleta hasara ya mabilioni ya pesa kwa uchumi wa dunia.

    Wawakilishi wa mashirika mbalimbali ya kibinadamu kama UNICEF na WFP wanatarajiwa kushiriki kwenye mkutano huo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako