• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mjumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia ataka majimbo yanayopingana kutekeleza makubaliano ya kusitisha vita

    (GMT+08:00) 2016-11-14 09:14:50

    Mjumbe wa Umoja wa mataifa nchini Somalia Bw. Michael Keating ametaka majimbo mawili yayopambana nchini humo kuheshimu na kutekeleza makubaliano ya kusitisha mapigano, ili kukomesha mapambano yaliyosababisha vifo vya watu wasiopungua 45.

    Bw Keating amesema ahadi zilizotolewa na Rais Abdiweli Mohamed Ali "Gaas" wa Puntland, na Abdikadir Hussein Guled wa Galmudug yanaridhisha, lakini ni lazima ziendane na utekelezaji kamili wa makubaliano.

    Taarifa ya Bw Keating inakuja baada ya mazungumzo yaliyofanyika mjini Galkayo na kuhudhuriwa na viongozi wa Somalia ikiwa pamoja na waziri mkuu wake Bw. Sharmarke, wawakilishi wa jumuiya ya kimataifa, wakuu wa majimbo hayo mawili.

    Mapambano yaliyolipuka mjini Galkayo yamesababisha vifo vya watu 45 katika muda wa wiki sita, na kufanya watu elfu 90 kupoteza makazi yao.

    .

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako