Polisi nchini New Zealand wamethibitisha kuwa watu wawili wamefariki dunia baada ya tetemeko kubwa la ardhi lenye nguvu ya 7.5 kwenye kipimo cha Richter kulikumba eneo la mashariki mwa Kisiwa cha Kusini nchini humo. Waziri mkuu wa nchi hiyo John Key amesema idadi ya vifo huenda itaongezeka wakati tathmini ya hasara inaendelea. Wizara ya ulinzi wa kiraia na usimamizi wa hali ya dharura ya nchi hiyo, ilitoa tahadhari ya tsunami kwenye pwani ya mashariki baada ya tetemko hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |