Ligi Kuu ya England msimu wa 2016/2017 iliendelea tena jana kwa mchezo mmoja kuchezwa, Chelsea iliyo chini ya kocha wake Antonio Conte walisafiri hadi dimba la Riverside kucheza na wenyeji wao Middlesbrough katika mchezo wao wa 12 wa EPL.
Wakiwa Chelsea ugenini walifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 1-0, goli ambalo lilitiwa nyavuni na mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania mwenye asili ya Brazil Diego Costa dakika ya 41, kwa ushindi huo Chelsea wanashika usukani wa Ligi Kuu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |