Ripoti ya shirika la kupambana na UKIMWI la Umoja wa Mataifa UNAIDS iliyotolewa huko Windhoek, Namibia, inasema watu milioni 38 wanaishi na virusi vya HIV kote duniani. Watu hao ni pamoja na wanawake milioni 18 na watoto milioni 1.8 wenye umri chini ya miaka 15. Ripoti hiyo pia imesema, mwaka jana pekee watu zaidi ya milioni 2 waliambukizwa virusi vya HIV, na laki 1.5 kati yao ni watoto.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |