Marubani wa Shirika la ndege la Ujerumani Lufthansa wametangaza kuwa watafanya mgomo leo. Vyombo vya habari vya Ujerumani vimesema safari zaidi ya 800 za ndege za shirika hilo zimefutwa kutokana na mgomo huo, na kuathiri abiria wapatao laki 1. Wafanyakazi wa shirika la ndege la Eurowings lililoko chini ya shirika la Lufthansa jana walifanya mgomo katika viwanja vya Dusseldorf na Hamburg, ambapo safari 60 za ndege na abiria zaidi ya elfu 4 waliathiriwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |