Zaidi ya watu 10 wamepoteza maisha mjini Mogadishu baada ya bomu kulipuka katika eneo la soko karibu na chuo cha zamani cha jeshi la anga cha Somalia.
Kwa mujibu wa taarifa ya polisi imesema kuwa, bomu hilo limelipuka katika soko lenye shughuli nyingi na wahanga zaidi ni raia na bado idadi kubwa ya majeruhi haijatambulika.
Naye afisa wa polisi Ahmed Farah amesema, kikosi cha usalama cha Somalia kimekwisha wasili kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |