• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mkutano wa kilele kuhusu maji wafunguliwa Hungary

    (GMT+08:00) 2016-11-29 09:34:43

    Mkutano wa kilele kuhusu maji utakaofanyika kwa siku tatu ulifunguliwa jana mjini Budapest, Hungary na kujadili utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa yanayohusiana na maji.

    Rais Ader Janos wa Hungary amehutubia ufunguzi wa mkutano huo akisema maji ni raslimali adimu, na pia ni msingi wa usalama na amani.

    Naye katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Bw. Ban Ki-moon amepongeza mkutano huo na kusisitiza kuwa mageuzi kwenye usimamizi wa raslimali ya maji ni ya lazima ili kutimiza maendeleo endelevu, na mbinu bora za kushughulikia maji taka zinatakiwa kuenezwa katika nchi mbalimbali.

    Mkutano huo unaoandaliwa kwa pamoja na serikali ya Hungary na Baraza la maji duniani WWC unahudhuriwa na washiriki 1,800 kutoka nchi zaidi ya mia moja.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako