• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa Mataifa watoa wito wa kuhakikisha usambazaji wa misaada ya kibinadamu nchini Sudan Kusini

    (GMT+08:00) 2016-12-01 08:54:41

    Umoja wa Mataifa umetoa wito kwa pande zinazopambana nchini Sudan Kusini kuhakikisha misaada ya kibinadamu inafikishwa bila vikwazo kwa watu wenye mahitaji.

    Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini Bw Eugene Owusu ameeleza wasiwasi mkubwa juu ya vizuizi vinavyotokana na urasimu, na vikwazo kwenye njia za kufikisha misaada ya kibinadamu nchini humo.

    Inakadiriwa kuwa watu milioni 3 wamelazimika kukimbia makazi yao, wakiwemo watu milioni 1.1 waliokimbilia nchi za jirani, tangu kulipuka kwa mapambano kati ya vikosi vinavyomtii rais Salva Kiir na wafuasi wa aliyekuwa makamu wa rais Bw Riek Machar.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako