Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger anasema kuwa kiungo wa kati wa timu hiyo Mesut Ozil atawashangaza wakosoaji wake katika mechi inayofuata.
Ozil alikosolewa vibaya baada ya Arsenal kushindwa 2-1 na Manchester City. Lakini Wenger amesema kuwa Ozil kama wachezaji wengine shupavu katika timu yake amekuwa akichukua jukumu kubwa na hivyo basi hapaswi kulaumiwa sana.
Anasema kwamba tatizo la Arsenal kupoteza mechi hiyo ilikuwa kushindwa kudhibiti mchezo katikati ya uwanja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |