Tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 7.6 katika kipimo cha Richter limekumba maeneo ya kusini mwa Chile na kuzusha hofu ya kutokea kwa tsunami, lakini halijasababisha kifo chochote. Ofisi ya taifa ya hali ya dharura ya Chile ONEMI imeamuru wakazi wa sehemu za pwani wahamishwe, lakini baadaye iliondoa tahadhari ya tsunami. Hata hivyo imeripotiwa kuwa barabara moja ya mwendo kasi iliharibiwa kiasi na tetemeko hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |