Jordan imetangaza mpango wake kuwasaidia wakimbizi wa Syria katika kambi kubwa zaidi ya wakimbizi nchini humo wakati wa majira ya baridi. Shirika la habari la Jordan limesema hatua zitakazochukuliwa ni pamopja na kuwalinda wakimbizi kutoka hali ya dharura kama vile mvua kubwa na mafuriko. Maandalizi hayo yanafanywa na mashirika ya huko na ya kimataifa katika kambi ya Zaatari yenye wakimbizi elfu 80 kutoka Syria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |