Rais Uhuru Kenyatta ametoa salamu za pongezi za mwaka mpya kwa wakenya, na kusema ingawa mwaka jana Kenya ilikumbwa na changamoto ya ugaidi, ukosefu wa ajira na mgomo wa madaktari, wakenya wanatakiwa kuwa na imani na taifa lao.
Amesema wakenya wanapaswa kuendelea kuwa na dhamira ya kupambana na matarajio ili kufanya nchi yao iwe na utulivu na ustawi
Akizungumza kuhusu uchaguzi ujao, rais Kenyatta amesema, anatarajia wakenya watakuwa watulivu na mshikamano, na kutoathiriwa na makundi ya nje.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |