Uchunguzi mpya wa maoni uliofanywa na Kampuni ya Gallup umeonesha kuwa, zaidi ya nusu ya wamarekani wana mashaka juu ya uwezo wa rais mteule Donald Trump katika kutatua migogoro ya kimataifa, kutumia nguvu ya kijeshi kwa busara, au kuepuka kashfa kubwa katika utawala wake. Akilinganishwa na marais wa awali, asilimia 70 ya wamarekani walikuwa na imani na Barack Obama, George W Bush na Bill Clinton katika maeneo hayo kabla yao kuingia madarakani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |