• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri wa mambo ya nje wa China kufanya ziara ya kwanza kwa mwaka huu katika nchi tano za Afrika

    (GMT+08:00) 2017-01-03 19:14:58

    Waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi atafanya ziara katika nchi tano za Afrika zikiwemo Madagascar, Zambia, Tanzania, Jamhuri ya Kongo na Nigeria kuanzia tarehe 7 hadi 12 mwezi huu.

    Hii ni desturi ya waziri wa mambo ya nje wa China kufanya ziara ya kwanza kila mwaka barani Afrika, ambayo imedumu kwa miaka 20.

    Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Geng Shuang amesema mwaka huu ni mwaka wa kuendeleza kwa kina ushirikiano kati ya China na Afrika. Ziara hiyo ya Bw. Wang Yi itahimiza makubliano mbalimbali yaliyofikiwa na rais Xi Jinping wa China na marais wa nchi za Afrika kwenye mkutano wa kilele wa Baraza la Ushirikano la China na Afrika uliofanyika mwaka jana mjini Johannesburg, Afrika Kusini.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako