• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mbio za Dunia za Nyika 2017 kufanyika Kampala Uganda

    (GMT+08:00) 2017-01-09 09:02:28

    Mashindano ya Dunia ya Mbio za Nyika yanatarajiwa kufanyika nchini Uganda mwezi Machi mwaka huu huku timu mbalimbali za Afrika Mashariki ni miongozi mwa nchi zinazotarajia kupeleka timu katika mpambano huo.

    Washindi wa mbio za mwaka huu za dunia kwa wachezaji mmoja mmoja atapata dola za Marekani 30,000. Huku washindi wa pili kwa wanaume na wanawake kila mmoja ataondoka na dola 3,000.

    Kwa upande wa zawadi za kitimu, timu itakayoshinda itatwaa dola za Marekani 20,000 wakati ile ya pili itaondoka na dola 16,000 na hadi mshindi wa sita atapata zawadi. Washindi wa mbio za kupokezana vijiti wataondoka na kitita cha dola za Marekani 12, 000.

    Tayari Shirikisho la Riadha la Uganda (UAF) limetangaza kikosi cha wachezaji 49 akiwemo bingwa wa marathoni wa Olimpiki Stephen Kiprotich.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako