Kikosi cha tatu cha askari wa miguu wa kulinda amani wa China jana kimekamilisha mafunzo maalumu ya kulinda amani, hivyo kukidhi vigezo vinavyotambuliwa vya ulinzi wa amani vilivyotolewa na ujumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini.
Askari hao wamepata mafunzo kuhusu ulinzi wa wakimbizi, kanuni za mapambano na udhibiti wa msukosuko.
Baada ya kukamilishasha mafunzo hayo, askari wa kulinda amani wa China watatekeleza majukumu mbalimbali ikiwemo kufanya doria, kulinda maeneo yaliyotengwa, silaha, pamoja na kulinda kambi ya wakimbizi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |