Mkataba wa Messi unakamilika 2018 na anatarajia kupewa mkataba mpya huku ikiripotiwa huenda akapewa kitita cha pauni milioni 21 wanazopata Luis Suarez na Neymar.
La Liga huweka mkataba na kila klabu kuhusu matumizi yao kila mwanzo wa msimu, ambapo huzizuia bodi kutotumia zaidi ya asilimia 70 ya bajeti yake ya mapato. Mkataba wenye mishahara mikubwa waliyopatiwa Suarez na Neymar ambayo itakamilika 2021, huchukua kiwango kikubwa cha matumizi ya timu hiyo.
Messi mwenye umri wa miaka 29, anaripotiwa kupokea pauni milioni 19 na Grau anasema kuwa nyongeza yoyote lazima ifikiriwe sana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |