Wakati Droo ya Raundi ya 4 ya Kombe kongwe Duniani, FA CUP, imeshafanyika, Leo Jumatano zipo Mechi za Marudiano za Raundi ya 3 kwa zile Timu zilizoenda Sare.
Moja ya Timu hizo ni Vigogo Liverpool ambao walibanwa na Timu ya Daraja la chini Plymouth Argyle huko Anfield na kutoka 0-0 na sasa wanapaswa kwenda Ugenini kwa Timu hiyo ya Daraja la 4 ili kurudiana nao.
Mshindi wa Mechi hiyo atakuwa Nyumbani kucheza Mechi ya Raundi ya 4 na Wolverhampton Wanderers. Mechi za Raundi ya 4 ya FA CUP zitaanza Ijumaa Januari 27 kwa Mechi 1 tu kati ya Derby County na Mabingwa wa England Leicester City. Mabingwa Watetezi wa FA CUP, Manchester United wao watacheza Raundi ya 4 kwao Old Trafford na Wigan Athletic hapo Jumapili Januari 29.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |