• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa Kenya amteua kiongozi mpya wa Kamati ya kupambana na ufisadi

    (GMT+08:00) 2017-01-20 10:11:23
    Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amemteua askofu mkuu aliyestaafu Bw Eliud Wabukala kuwa kiongozi mpya wa Kamati ya kupambana na ufisadi nchini Kenya EACC kwa muda wa miaka mitano.

    Bw Wabukala atachukua nafasi ya Bw. Philip Kinisu anayelazimika kujiuzulu kutokana na familia yake kutuhumiwa kupokea dola milioni 7.91 za kimarekani kutoka kwa Shirika la kitaifa la huduma kwa vijana NYS.

    Taarifa ya bunge la Kenya imesema Rais Kenyatta amemtakia Bw. Wabukala kuwa na mafaniko kwenye wadhifa mpya, akisisitiza kuwa Bw. Wabukala ni kiongozi anayeaminika na kuheshimika, na ana uwezo wa kuongoza vizuri tume ya kupambana na rushwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako