Rais Paul Kagame wa Rwanda amesisitiza mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya mkakati wa kidigitali kwenye mkutano wa baraza la uchumi duniani WEF mjini Davos. Rais Kagame amesema ingawa serikali zinaweza kutoa mchango katika kuendeleza teknolojia ya kidigitali kwenye upande wa sera, sekta binafsi pia inahitajika kama mwenzi kwenye uvumbuzi na uwekezaji. Amesema ana imani kuwa Afrika inayojiendeleza kutoka kwenye msingi wa chini, inalenga kujiendekeza haraka, kwa kutambua kuwa teknolojia ya mawasiliano ya habari ina manufaa zaidi kuliko hatari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |