• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kasi ya ongezeko la Pato la taifa la China yashuka hadi chini zaidi katika miaka 26 iliyopita lakini kutimiza lengo la serikali.

    (GMT+08:00) 2017-01-20 19:55:16

    Takwimu rasmi zilizotolewa leo na Idara ya Takwimu ya Taifa ya China zinaonesha kuwa mwaka jana uchumi wa China ulikua kwa asilimia 6.7, ikiwa ni kasi ndogo zaidi ya ongezeko katika miaka 26 iliyopita, lakini inaendana na lengo lililowekwa na serikali.

    Kwa mujibu wa Idara hiyo, pato la taifa la China lilifikia dola za kimarekani trilioni 10.83, huku sekta ya huduma ikichukua asilimia 51.6.

    Takwimu hizo pia zinaonesha kuwa viashiria vikuu vya kiuchumi vililegea mwaka jana, ambapo ongezeko la uzalishaji wa kiviwanda lilipungua hadi kwa asilimia 6 kutoka asilimia 6.1 ya mwaka 2015.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako