Jeshi la usalama la Iraq limetwaa maeneo mengine katika sehemu ya katikati mashariki mwa Mosul, huku likiendelea kupambana na kundi la IS na kulitimua kundi hilo kutoka ngome yao ya mwisho katika kitongoji cha kaskazini mwa mji huo. Kamanda mmoja wa operesheni za pamoja ametoa taarifa akisema vikosi vya Iraq vimetwaa maeneo mawili ya katikati ya mji wa Mosul na kupeperusha bendera ya taifa kwenye baadhi ya majengo ya maeneo hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |