Rais Donald Trump wa Marekani amesema kuwa Marekani itaanza mazungumzo tena na Mexico na Canada kuhusu makubaliano ya biashara huria ya Amerika kaskazini.
Rais Trump amesema kwenye sherehe ya kuapishwa kwa msaidizi mwandamizi wa Ikulu ya Marekani kuwa atakutana na viongozi wa Mexico na Canada hivi karibuni na kujadili masuala ya biashara.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani Bw. Seam Spicer hivi karibuni alisema rais Trump atakutana na rais wa Mexico na kujadili masuala ya makubaliano ya biashara huria na suala la uhamiaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |