• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Konta uso kwa uso na Serena michuano ya wazi ya Tenisi (Australian Open)

    (GMT+08:00) 2017-01-24 08:53:09

    Mcheza tenisi wa Uingereza, Johanna Konta ametinga robo fainali ya mashindano ya wazi ya Australia, baada ya kumtoa Mrusi Ekaterina Makarova kwa jumla ya 6-1 6-4, huko Melbourne Park, mjini, Melbourne.

    Konta mwenye umri wa miaka 25, sasa atakutana na kigogo wa tenesi Mmarekani, Serena Williams ambaye naye ameshinda 7-5 6-4 dhidi ya Barbora Strycova kutoka Jamhuri ya Czech.

    Naye Mcroatia Mirjana Lucic-Baroni alimaliza kiu yake ya kusubiri kwa miaka 18 kutinga robo fainali kwa mashindano ya Gland Slam, baada ya kupata ushindi dhidi ya Mmarekani Jennifer Brady

    Lucic-Baroni, mwenye umri wa miaka 34, alishinda kwa seti mbili za 6-4 6-2 na kutinga robo fainali kwa mara ya kwanza tangu atolewe na Steffi Graf kwenye mashindano ya Wimbledon mwaka 1999.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako