Mcheza tenisi wa Uingereza, Johanna Konta ametinga robo fainali ya mashindano ya wazi ya Australia, baada ya kumtoa Mrusi Ekaterina Makarova kwa jumla ya 6-1 6-4, huko Melbourne Park, mjini, Melbourne.
Konta mwenye umri wa miaka 25, sasa atakutana na kigogo wa tenesi Mmarekani, Serena Williams ambaye naye ameshinda 7-5 6-4 dhidi ya Barbora Strycova kutoka Jamhuri ya Czech.
Naye Mcroatia Mirjana Lucic-Baroni alimaliza kiu yake ya kusubiri kwa miaka 18 kutinga robo fainali kwa mashindano ya Gland Slam, baada ya kupata ushindi dhidi ya Mmarekani Jennifer Brady
Lucic-Baroni, mwenye umri wa miaka 34, alishinda kwa seti mbili za 6-4 6-2 na kutinga robo fainali kwa mara ya kwanza tangu atolewe na Steffi Graf kwenye mashindano ya Wimbledon mwaka 1999.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |