Mazungumzo ya Astana kuhusu mgogoro wa Syria yaliyofanyika kwa siku mbili, yamemalizika na kutoa taarifa ya pamoja ikiunga mkono usimamishaji vita wa mwaka mmoja, na kwa mara ya kwanza kuwakutanisha uso kwa uso mahasimu wa pande zinazopambana.
Russia, Uturuki na Iran nchi zilizofadhili mazungumzo hayo zimetoa taarifa ikisisitiza kuheshimu mamlaka, uhuru, umoja na ukamilifu wa ardhi ya Syria. Pande hizo zimesema zinaunga mkono mazungumzo kati ya serikali ya Syria na wapinzani, na kuona kuwa hakuna suluhisho la kijeshi kwenye mgogoro wa Syria. Hata hivyo zimesema zitaendelea kutoa msaada kwenye mapambano dhidi ya makundi ya kigaidi ya IS na Nusra Front.
Mkutano huo pia umeimarisha makubaliano ya kusimamisha vita yaliyofikiwa mwishoni mwa mwaka jana
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |