• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Vikosi vya Umoja wa Afrika vyatwaa tena mji wa Badade kutoka kwa Kundi la Al-Shabaab

    (GMT+08:00) 2017-01-25 09:15:33
    Tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM imesema vikosi vyake na vya jeshi la Somalia vimetwaa tena mji wa Badade, kusini mwa Somalia uliokuwa unadhibitiwa na Kundi la Al-Shabaab.

    Taarifa iliyotolewa jana na AMISOM imesema jeshi la pamoja limewashambulia vikali wapiganaji wa Al-Shabaab katika operesheni hiyo iliyofanywa mapema jana, ambapo wapiganaji hao walijaribu kujibu mashambulizi ili kuteka tena mji wa Badade.

    Badade ni mji muhimu wa pwani katika eneo la Lower Juba, kusini mwa Somalia, ambao ulidhibitiwa na wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab baada ya vikosi vya Kenya kuondoka mwezi Januari mwaka jana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako