• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Watu 13 wauawa kwenye shambulizi la kujitoa muhanga Afghanistan

    (GMT+08:00) 2017-02-08 09:31:26

    Shambulizi la kujitoa muhanga dhidi ya mahakama Kuu ya Afghanistan, lililotokea jana mjini Kabul limesababisha vifo vya watu 13 na wengine 25 kujeruhiwa.

    Shambulizi hilo lilitokea jioni wakati wafanyakazi walipokuwa wakitoka kazini, ni la pili dhidi ya mahakama hiyo katika muda wa miaka mitatu. Hadi sasa hakuna kundi lililotangaza kuhusika na shambulizi hilo.

    Wizara ya afya ya Afghanistan imethibitisha kutokea kwa vifo hivyo, na kusema watu 41 waliojeruhiwa wamepelekwa hospitali. Lakini mashuhuda wamesema idadi ya vifo na majerahi ni kubwa kuliko iliyotangazwa.

    Umoja wa Mataifa umelaani vikali shambulizi hilo na kutoa rambirambi kwa familia za wahanga na kwa serikali ya Afghanistan.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako