India imeweka rekodi mpya kwa kuwa nchi iliyorusha satilaiti nyingi kwa wakati mmoja baada ya leo asubuhi kufanikiwa kurusha satilaiti 104 kwa pamoja.
Rekodi ya awali iliwekwa na Russia mwaka 2014, ambayo ilirusha satilaiti 37 kwa wakati mmoja.
Kati ya satilaiti hizi ambazo nyingi zinamilikiwa na wateja wa kimataifa, moja muhimu zaidi ni ile ya kuchunguza sayari ya dunia ya India ambayo ina uzito wa kilo 714, na nyingine nyingi ambazo satilaiti ndogo ndogo zinazomilikiwa na Marekani, Israel, Kazakhstan, Uholanzi, Uswisi, na Falme za Nchi za Kiarabu
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |