Mwanariadha wa Rwanda, Joseph Areruya jana aliwezesha nchi yake kushinda medali ya shaba kwenye mashindano ya riadha ya mabingwa bara la Afrika yanayoendelea mjini Luxor Misri.
Aureruya alimaliza katika nafasi ya 4 baada ya kutumia dakika 55 sekunde 56 na kuonysha kuwa kiwango chake kimepanda kuliko mwaka 2016 aliposhiriki mashindano kama haya.
Nae mwanariadha Stefan Debod wa Afrika Kusini kushinda medali ya dhahabu baada ya kumaliza katika nafasi ya kwanza baada ya kutumia dakika 53 na sekunde 42, wakati Hebtom Awet kutoka Eritrea alishinda medali ya fedha baada ya kumaliza katika nafasi ya pili kwa kutumia dakika 54 na sekunde 5.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |