Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang jana alikutana na mwenzake wa Ufaransa Bw. Bernard Cazeneuve hapa Beijing. Kwenye mazungumzo yao Bw. Li Keqiang amesema, China inapenda kuimarisha ushirikiano na Ufaransa kwenye sekta za nishati ya nyuklia, usafiri wa anga, kilimo, matibabu na uhifadhi wa mazingira. Bw. Cazeneuve amesema Ufaransa inapenda kushirikiana na China katika sekta mbalimbali, na pia inapenda kufanya juhudi pamoja na China kulinda uhuru wa kibiashara na kuondoa sera za kujilinda kibiashara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |