Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe aliyetimiza umri wa miaka 93 hivi karibuni ambaye pia ni katibu mkuu wa chama tawala cha ZANU-PF, amesema kwa sasa hatateua mwenyekiti ajaye wa chama hicho, na kwamba uteuzi huo utafanyika kwenye mkutano wa chama utakaofanyika mwaka 2019.
Akizungumzia suala la uteuzi huo, rais Mugabe amesema vitendo vyote vya chama vinaamuliwa na katiba ya chama, ambayo inaelekeza kuwa mwenyekiti wa chama anatakiwa kuteuliwa kwenye mkutano wa wanachama badala ya kuteuliwa naye.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |