• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya yamaliza sensa maalum ya wanyamapori

    (GMT+08:00) 2017-02-28 18:28:40

    Shirika la Huduma kwa Wanyamapori nchini Kenya KWS limemaliza sensa maalum ya wanyamapori waishio katika mpaka wa Kenya na Tanzania.

    Msemaji wa KWS Paul Gathitu amesema sense hiyo imefanywa kwa ajili ya kufahamu idadi ya wanyamapori, njia wanazopita, maji na rasilimali za nyanda za malisho, na kwamba ripoti kamili itatolewa mwezi ujao.

    Naibu mkurugenzi wa KWS anayeshughulikia usimamizi wa ikolojia Shadrack Ngene amesema kazi hiyo itasaidia juhudi za kuwalinda Ndovu na wanyamapori wengine na kukabiliana na matishio mbalimbali kama vile shughuli za binadamu na mabadiliko ya hali ya hewa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako