Omar al-Bashir, amteuwa makamu wake kuwa waziri mkuu
Rais wa Sudan, Omar al-Bashir, amemteuwa makamu wake wa rais Bakri Hassan Saleh kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo.
Bwana Saleh ni mmoja wa mshirika wa karibu zaidi wa Bashir, na alihusika katika mapinduzi ya mwaka 1989 yaliyomleta mamlakani Omar Al Bashir.
Huku wakiwa chini ya shinikizo kali kutoka kwa upinzani na jamii ya kimataifa, Bwana Mr Bashir amebuni cheo cha waziri mkuu, ambacho aliifutilia mbali mara tu baada ya kuingia uongozini kwa njia ya mapinduzi.
Rais wa Gambia afanya ziara ya kiserikali nchini Senegal
Rais wa Gambia Adama Barrow amefanya ziara ya kiserikali nchini Senegal Alhamisi wiki hii, kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano kwenye Ofisi ya rais wa Senegal Hamidou Elhadji Kassé.
Bw Barrow aliwasili mjini Dakar Alhamisi wiki hii saa 4:00 asubuhi (saa za Afrika Magharibi).
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |