Rais wa Gambia Adama Barrow alikutana kwa mazungumzo na mwenzake wa Senegal Macky Sall Alhamisi mchana.
Kwa mujibu wa Ofisi ya rais wa Senegal, Bw Barrow atafanya ziara binafsi Ijumaa kwa viongozi wa kidini.
Mikataba ya ushirikiano wa kiuchumi na kidiplomasia itasainiwa siku ya Jumamosi.
Adama Barrow alichaguliwa kuwa rais wa Gambia tarehe 1 Desemba 2015, lakini mtangulizi wake Yahya Jammeh alikataa kuondoka madarakani baada ya kukubali awali kushindwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |