Refa Michael Oliver alizungukwa na wachezaji wa United baada ya kumpa kadi nyekundu Ander Herrera dakika 10 kabla ya muda wa mapumziko. United ilipoteza mechi hiyo kwa 1-0. Taarifa ya FA iliipa United hadi saa kumi na mbili jioni jana kwa saa za Uingereza kujibu.
Kiungo wa kati wa Uhispania Herrera alitolewa nje baada ya kumchezea vibaya kwa mara ya pili mshambuliaji Eden Hazard. Hakuna hatua zaidi itakayochukuliwa dhidi ya Marcos Rojo akwa kosa alilofanya katika dakika za mwisho za mechi. Rojo alionekana akimkanyaga Hazard.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |