Idadi ya vifo kutokana na maporomoko ya lundo la taka pembezoni mwa Addis Ababa nchini Ethiopia imefikia 113, ambapo nchi hiyo iliingia kwenye kipindi cha maombolezo ya taifa cha siku tatu. Ofisi ya habari ya serikali ya Addis Ababa imesema waokoaji walipata miili 41 kwenye eneo la tukio, na kufanya idadi ya jumla ya vifo kufikia 113, wengi wao wakiwa ni wanawake. Ofisi hiyo pia imesema huenda idadi hiyo ikaongezeka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |