Ethiopia imewapongeza na kuwatuza wakulima katika juhudi zao za kukuza uzalishaji na kuboresha kipato.
Waziri mkuu Hailemariam Dessalegn ametoa tuzo 570 kwa wakulima wa sekta mbali mbali kwa kutambua harakati zao za kuimarisha sekta ya kilimo na kuvutia wawekezaji nchini humo.
Hii ni baada ya idadi ya wakulima kuongeza baada ya wafugaji wa kuhamahama kujiotoa katika kilimo hicho na kuingia kwenye kilimo cha mimea.
Yenesew Adugna kutoka chama cha wakulima cha wanawake Ethiopia amesema wamepokea mtaji wa biir milioni 1.5 kwa wanacahama kadhaa ambazo zitatumika kuboresha kilimo kwa kupata mbegu bora na mbolea nafuu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |