• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania Majaliwa akaribisha Irani kuwekeza katika kilimo,uvuvi

    (GMT+08:00) 2017-03-20 19:37:57

    WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewakaribisha wawekezaji kutoka nchini Iran kujitokeza kuwekeza kwenye viwanda mbalimbali vikiwemo vya kuchakata mazao ya kilimo na uvuvi nchini Tanzania.

    Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo alipokutana na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mousa Farhang jijini Dar es Salaam.

    Alisema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kujenga uchumi wa viwanda ili kuongeza ajira na kuondoa umasikini miongoni mwa wananchi wake, hivyo wanahitaji uwekezaji mkubwa kwenye sekta mbalimbali.

    Pia Waziri Mkuu aliwakaribisha raia wa Iran kuitembelea Tanzania kama watalii kwa sababu kuna fursa nyingi za utalii ukiwemo Mlima wa Kilimanjaro ambao unaongoza kwa urefu barani Afrika pamoja na mbuga nyingi zilizosheheni wanyama.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako