Ratiba ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika imetoka, na timu 16 zilizotolewa katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika sasa kukutana katika kinyang'anyiro cha kombe la Shirikisho. Washindi 16 wa Raundi hiyo watacheza hatua ya makundi.
Droo ya raundi ya mchujo ya kombe la Shirikisho imefanyika Makao Makuu ya CAF Jijini Cairo nchini Misri. Droo hii imekutanisha timu 16 zilizoshinda raundi ya kwanza ya Mashindano haya na kupambanishwa na timu 16 zilizotupwa nje ya raundi ya kwanza ya CAF champions ligi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |