Umoja wa Mataifa unatarajiwa kupanua operesheni zake za kukabiliana na ukame nchini Somalia, baada ya kupitisha mkopo wa dola milioni 22 za kimarekani kwa nchi hiyo. Naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw Stephen O'Brien amesema zaidi ya watu milioni 2.9 nchini Somalia wanakabiliwa na hatari ya njaa, na huenda wengi watakufa njaa kama hatua madhubuti hazitachukuliwa. Bw. O'Brien amesema, mkopo huo utaliwezesha Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO kutoa misaada ya dharura nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |