Golikipa namba moja wa klabu ya Arsenal, Peter Cech ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa Jamhuri ya Czech kwa mwaka 2016. Hii ni mara ya 9 mchezaji huyo kushinda hiyo tuzo. Cech ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 34, ameshastaafu kuichezea timu ya taifa ya Jamhuri ya Czech tangu mwaka jana baada ya michuano ya Euro nchini Ufaransa. Amestaafu akiwa ameichezea timu hiyo mechi 124.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |