• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Marc Wilmots atangazwa kuwa kocha mpya wa Ivory Coast

    (GMT+08:00) 2017-03-23 08:46:37

    Kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Ubelgiji, Marc Wilmots ametangazwa kuwa kocha mpya wa Ivory Coast.

    Wilmots mwenye miaka 48, ametangazwa Jumanne hii na shirikisho la soka la nchini humo (FIF) kuwa kocha wa timu hiyo akichukuwa nafasi ya Michel Dussuyer ambaye alijiuzulu mwezi Februari mwaka huu baada ya timu hiyo kutolewa katika hatua ya makundi ya kombe la mataifa ya Afrika yaliyofanyika nchini Gabon.

    Marc alifanikiwa kuifikisha Ubelgiji kwenye hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la dunia 2014 iliyofanyika Brazil na hatua ya nane bora ya michuano ya Uefa Euro mwaka jana.

    Kocha huyo atakuwa na kibarua cha kuhakikisha timu ya Ivory Coast inafuzu kucheza kombe la dunia mwakani nchini Urusi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako