Benki ya Standard Chartered imepata ongezeko kubwa zaidi la faida miongoni mwa benki zote nchini Kenya katika mwaka wa 2016.
Benki hiyo imepata ongezeko la faida la asilimia 42.7 sawa na bilioni 9.05 na imetangaza kwamba itatoa mgao wa faida kwa wana hisa wake wa shilingi 14 kwa kila hisa.
Mwaka wa 2015, Stanchart ilipata faida ya shilingi bilioni 6.34.
Mapato ya mwaka 2016 yameongezeka kutokana na kupungua kwa utoaji wa mikopo kwa asilimia 55.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |