Mashindano ya mbio za nyika yamemalizika mjini Kampala Uganda yakishuhudiwa wanariadha toka Kenya na Ethiopia wakiendelea kutawala katika riadha duniani.
Katika mbio hizo, wanariadha wa Kenya, Uganda, Ethiopia na Uturuki walitawala na kunyakua medali zote, huku wanariadha wa Tanzania wakiwa wasindikizaji.
Nafasi ya juu iliyopata Tanzania katika mbio hizo ni pale ilipoambulia nafasi ya nane katika mbio za kupokezana vijiti za kilomita nane.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |