• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Ligi kuu ya Uingereza (EPL) kuendelea April, Manchester United shughuli pevu

    (GMT+08:00) 2017-03-29 09:33:17

    Baada ya kukaa pembeni kwa wiki mbili kupisha mechi za kimataifa, Manchester United wanarudi kilingeni Jumamosi Aprili 1 kwa kucheza nyumbani mechi ya ligi kuu England, dhidi ya West Bromwich Albion Uwanjani Old Trafford.

    Mechi hiyo ni mwanzo wa mfululizo wa mechi 9 ambazo watazicheza mwezi Aprili na 7 kati ya hizo ni za EPL wakati 2 ni za UEFA EUROPA Ligi za robo fainali wakipambana na klabu ya Belgium Anderlecht.

    Hivi sasa Man United wapo nafasi ya 5 kwenye ligi wakiwa na Pointi 52 kwa mechi 27 wakiwa nyuma ya timu ya 4 Liverpool kwa Pointi 2 lakini Liverpool wamecheza Mechi 2 zaidi yao wakati timu ya 3, Man City, wakiwa mbele yao kwa Pointi 5 lakini nao wamecheza mechi 1 zaidi yao.

    Timu ya Pili ni Tottenham wenye pointi 59 kwa mechi 28 na vinara ni Chelsea wenye pointi 69 kwa mechi 28.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako