Waziri wa mambo ya nje wa Kenya Bibi Amina Mohamed amesema, wakenya wanne ni kati ya wafanyakazi sita wa misaada waliouawa wakati msafara wao uliposhambuliwa jumamosi iliyopita.
Bibi Amina Mohamed amesema wakenya hao wanne walikuwa wanafanyakazi wa GREDO, ambalo ni shirika lisilo la kiserikali linalofadhiliwa na shirika la kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNICEF kujenga vituo vya vijana huko Pibor.
Amesema idara ya usalama ya Sudan Kusini inafanya juhudi ikishirikiana na maofisa kutoka Shirika la GREDO na UNICEF kurejesha miili yao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |