Nege ya kwanza ikiwa na abiria 49 ilitua kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta Jumatano.
Awali ndege zote za kibiashara kutoka Mogadishu zilitakiwa kwanza kutua mjini Wajir kwa ukaguzi wa kiusalama.
Kurejeshwa kwa safari hizo kunafuatia ziara aliyofanya nchini Kenya rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Farmajo.
Waziri wa usalama nchini Kenya Jospeh Nkaisery amesema wataendelea kuhakikisha ndege zote kutoka Somalia zinakaguliwa ili kudumisha hadhi ya kimataifa ya kiusalama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |