Kampuni ya kutengeneza magurudumu ya magari Sameer Africa imetangaza kwamba ilipata hasara ya shilingi milioni 877 kufuatia kufungwa kwa kiwanda chake mwaka jana.
Imesema kwamba kupanga upya oparesheni zake na kufungwa kwa kiwanda kumeilazimu kutumbukia kwenye hasara.
Sameer ilifunga kiwanda chake mwaka jana Agosti ikilalamikia mazingira mabaya ya kibiashara ikiwemo kuigizwa kwa magurudumu ya bei rahisi kutoka nchi za nje na kupanda kwa gharama ya uzalishaji.
Sasa kampuni hiyo inapanga kuanza kuuza magurudumu yanayotengenezewa nje ya nchi, kukondisha kiwanda chake na kuwekeza kwenye ujenzi wa nyumba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |